Rais Jakaya Kikwete amefanya uteuzi wa Makatibu Wakuu watano wapya na kuwahamisha wengine wanne kutoka wizara moja kwenda nyingine.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, uteuzi na uhamisho huo unaanza mara moja.
Taarifa hiyo imeeleza kwamba mabadiliko hayo yametokana na muundo mpya wa Serikali ambako Wizara ya Miundombinu imegawanywa katika wizara mbili, na baadhi ya Makatibu Wakuu kustaafu kazi kwa mujibu wa sheria.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Rais Kikwete amemteua Fanuel E. Mbonde kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Ikulu. Kabla ya uteuzi Mbonde alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu.
Wengine walioteuliwa ni Hussein Kattanga - Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa; John M. Haule - Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Herbert Mrango - Wizara ya Ujenzi na Eric K. Shitindi - Wizara ya Kazi na Ajira.
Kabla ya uteuzi wake Kattanga alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Haule alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Mrango alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi , Shittindi alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma.
Kwa upande wa waliobadilishwa vituo vyao, Rais Kikwete amemhamisha Sazi Salula kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwenda Ofisi ya Makamu wa Rais, Maimuna Tarishi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu kwenda Wizara ya Maliasili na Utalii.
Pia Injinia Omar Chambo anahamia Wizara ya Uchukuzi akitokea Wizara ya zamani ya Miundombinu na Kijakazi Mtengwa -anakuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.
Taarifa ilieleza kwamba kuwa Dk. Ladislaus Komba, aliyekuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii anapangiwa kazi maalum katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Aidha, Rais Kikwete amemhamishia Elizabeth Nyambibo Wizara ya Fedha na Uchumi ambako anachukua nafasi ya Naibu Katibu Mkuu iliyoachwa wazi na Haule. Kabla ya uhamisho Nyambibo alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo Makatibu Wakuu wanatarajia kuapishwa leo saa tatu Machi
00000